Sunday, 25 May 2014

SAUTI ZA UASI ZIMEKUWEPO




Sauti za uasi zimekuwepo 

Sauti za uasi zimekuwepo, msijitie bashasha zenu sio za kwanza

Tazameni uasi huu wa kipepo, magauni na surwali ndo wameongeza

Msidanganyike ati ni maedeleo, kumbukeni Edeni baada yao kudanganywa

Mungu alishutumiwa na kufanywa chukizo, ati asingelipenda wawe kama Mola

 

Sauti za uasi zimekuwepo, msijitie bashasha zenu sio za kwanza

Maendeleo mmeifanya nduano, mithili Nimrodi Babeli kujenga

Vyeti na mashahada mmejaza mifuko, waja kuwatisheni ati hekima imewakolea

Wale dhaifu shabaha ya venu vitisho, ila waadilifu twajua  kingo za wenu ujanja

 

Sauti za uasi zimekuwepo, msijitie bashasha zenu sio za kwanza

Babenyu ni yule mwongo, shaitwani mwingi wa kibri na shutma

Kabla ya ulimwengu kuwepo, hatiani Mola kampata 

Kazua uzushi kijitakia cheo, enzi aimiliki kana kwamba ndiye Mumba

 

Sauti za uasi zimekuwepo, msijitie bashasha zenu sio za kwanza

Uhuru wa kujieleza twajua upo, msifyate midomo twa wahimiza

Ukombozi pia upo, katu Injili hamwezi ilemaza

Japo giza kawa totoro, nuru ya Injili kote itaangaza

 

Sauti za uasi zimekuwepo, msijitie bashasha zenu sio za kwanza

Matusi mwazidisha kila uchao, ila hamtafanikiwa imani kudhalalisha

Hadhara tahadhari yao maelezo, maana mwana wa nyoka daima ni nyoka

Uasi kweli ni uozo wala sio maendeleo , ila laana sitowaombea bali neema inayookoa