Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Enyi aila yake Mungu wa kweli, Muumba wa mbingu, dunia, ulimwengu na vyote vilivyomo, natuishikeni itikadi yetu ya Ukristo kwa kumtukuza Mungu kwanza:- Daima mwaminifu na daima mkweli, ndani yake hamna hila wala hata chembe cha uovu hakiwezi patikana karibu ya uvuli wake, kwa kuwa Ewe, ni nuru na mwanga wala hamna hata giza katika uvuli wake. Ndiye aangazaye njia na kutuelekeza sote kwa mapito yaliyonyooka ambayo huishia uzima wa milele. Amin.
Wapendwa, kwa neema yake Mungu Baba katika Kristo Yesu, leo hii tutaendeleza mada tuliyoianza wiki jana ya kujifahamisha nyakati na misimu. Natumai sote twafahamu umuhimu wa kujua na kuelewa vema nyakati, hususan msimu tunaoishi ili tusipatikane kama wanawali walioishiwa na mafuta wakati bwana harusi alipochelewa kuja au kama mtumwa aliyetelekeza majukumu yake, (MT. 25:1-13; LK. 12:42-46). Siku zote wateule wa Mungu, yatupasa kuwa tayari kumpokea Bwana wetu maana yeye mwenyewe atuonya kuwa yuaja kama mwizi wakati hakuna mtu anamkusudia, (LK. 12:35-40). Basi tuweni waangalifu kwa kukesha tukiomba na kulisoma Neno Lake daima ili tupatikane tayari na wastahiki wa kuingia karamuni naye tamanio la moyo wetu, Bw. Yesu Kristo.
Wiki jana, tuliangazia vipindi vitatu vya kwanza na hapa ndipo tutachukulia na kuangazia vipindi viwili kama inavyofuata;
SIKU YA NNE
(MWA. 1:14-19)
HISTORIA YA ULIMWENGU
KANISA LA THIATIRA
(UFU. 2:18-29)
Siku hii inafananishwa na
kipindi cha Uangazo.
Kipindi hiki kilishuhudia
umoja na ushirikiano wa kanisa ukigawanyika kuwa madhehebu mawili; Ukatoliki
na Uprotestanti. Isitoshe, mamlaka na elimu zikatofautishwa baina yale ya
dini na ya ulimwengu. Migawanyiko hii kupitia madhehebu yake madogo madogo
pamoja na mashule na vyuo vya kila aina, ikaeneza nuru kote duniani. Wanadamu
wakila-tabaka na kila nchi duniani wakafikiwa na dini pamoja na elimu.
Sawa na mianga ile miwili
ambayo Mungu aliifanya pamoja na nyota, vyote vitie nuru juu ya nchi na
kutenga nuru na giza.
Katika Agano la Kale kipindi hiki
utambulika kuwa kile ambacho kilifuatia kuaga kwa Mfalme Suleimani ambapo Taifa
la Israeli liligawanyika mara mbili, kukawa na Israeli upande wa Kaskazini na
Yuda upande wa kusini. Wakati huu, Mungu akawainuilia manabii waangaze nuru
ya neno lake kwa watu wake ili kuwatenganisha na giza ya maovu waliotenda
sawa na mataifa mengine.
Kipindi hiki kilianza na mgawanyiko wa
umoja wa Kanisa uitwao “Reformation” na
kuendelea wakati wa “Industrial
Revolution” hadi kumilikiwa kwa mataifa madogo na yale yenye uwezo
(ukoloni).
Kanisa la msimu huu lilitambulika kwa
matendo, imani, huduma na subira. Maana katika kipindi hiki ndipo watu wengi
walijitolea maisha ya utawa na umishonari kuenenda wasipokujua kulihubiri
Injili. Wegine wakijitolea kwa huduma mbali-mbali kwa hali na mali aidha
kufadhili, kuasisi na kundikwa kazi hata kujiunga pasi na kutarajia malipo yo
yote.
-Lilitambulika kwa matendo, imani, huduma
na subira.
-Mgawanyiko kwa mafunzo ya Yezebeli Nabii
wa uwongo aliyefunza, kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu na uzinzi
-Bwana naye awaapia hukumu wale wakosaji
na urithi wa mamlaka ya kutawala mataifa kwa fimbo ya chuma kwa wale
waaminifu.
SIKU YA NNE
(MWA. 1:14-19)
HISTORIA YA ULIMWENGU
KANISA LA THIATIRA
(UFU. 2:18-29)
Siku hii inafananishwa na
kipindi cha Uangazo.
Kipindi hiki kilishuhudia
umoja na ushirikiano wa kanisa ukigawanyika kuwa madhehebu mawili; Ukatoliki
na Uprotestanti. Isitoshe, mamlaka na elimu zikatofautishwa baina yale ya
dini na ya ulimwengu. Migawanyiko hii kupitia madhehebu yake madogo madogo
pamoja na mashule na vyuo vya kila aina, ikaeneza nuru kote duniani. Wanadamu
wakila-tabaka na kila nchi duniani wakafikiwa na dini pamoja na elimu.
Sawa na mianga ile miwili
ambayo Mungu aliifanya pamoja na nyota, vyote vitie nuru juu ya nchi na
kutenga nuru na giza.
Katika Agano la Kale kipindi hiki
utambulika kuwa kile ambacho kilifuatia kuaga kwa Mfalme Suleimani ambapo Taifa
la Israeli liligawanyika mara mbili, kukawa na Israeli upande wa Kaskazini na
Yuda upande wa kusini. Wakati huu, Mungu akawainuilia manabii waangaze nuru
ya neno lake kwa watu wake ili kuwatenganisha na giza ya maovu waliotenda
sawa na mataifa mengine.
Kipindi hiki kilianza na mgawanyiko wa
umoja wa Kanisa uitwao “Reformation” na
kuendelea wakati wa “Industrial
Revolution” hadi kumilikiwa kwa mataifa madogo na yale yenye uwezo
(ukoloni).
Kanisa la msimu huu lilitambulika kwa
matendo, imani, huduma na subira. Maana katika kipindi hiki ndipo watu wengi
walijitolea maisha ya utawa na umishonari kuenenda wasipokujua kulihubiri
Injili. Wegine wakijitolea kwa huduma mbali-mbali kwa hali na mali aidha
kufadhili, kuasisi na kundikwa kazi hata kujiunga pasi na kutarajia malipo yo
yote.
-Lilitambulika kwa matendo, imani, huduma
na subira.
-Mgawanyiko kwa mafunzo ya Yezebeli Nabii
wa uwongo aliyefunza, kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu na uzinzi
-Bwana naye awaapia hukumu wale wakosaji
na urithi wa mamlaka ya kutawala mataifa kwa fimbo ya chuma kwa wale
waaminifu.
SIKU YA TANO
(MWA. 1:20-23)
HISTORIA YA ULIMWENGU
KANISA LA SARDI
(UFU. 3:1-6).
Siku hii inafananishwa na
kipindi cha Madhila.
Kipindi hiki kimejaa ubishani,
fujo na mashindano. Kila mtu akitaka
kuitawala nafsi yake mwenyewe. Desturi za Ukristo hazi heshimiki wala kutambuliwa, uasi Mungu
umekidhiri mpaka ndani ya Kanisa. Wanadamu wanajishugulisha na haja zao za
mwili peke yake kwa hivyo dhambi imezidi
hata kupita mipaka. Kwa Kanisa, madhila makuu ya ungojea mwili wa
Kristo, maana, dhambi inatawala kote hata Kanisani jambo ambalo Mwenyezi atarekebisha
mwenyewe na kuutakasa Mwili wa Kristo na ulimwengu kwa hukumu za
kutisha.
Sawa na wanyama ambao Mungu aliwafanya katika siku hii,
kila mmoja huitawala nafsi yake na kuongozwa na tamaa zake. Ndivyo ulimwengu
ulivyo katika enzi hii.
Katika Agano la Kale kipindi hiki kilianza
na utawala wa Mfalme Manase. Utawala kuwa umejaa kila aina ya maovu na
madhila kiasi cha kumkasirisha Mungu. Kinpindi hiki kiliendelea hadi pale
wana wa Israeli walipoharibiwa na adui zao na kubebwa mateka hadi Babloni.
Kipindi hiki kilianza na vita vya Kwanza vya Dunia. Ambavyo vilichangia pakubwa kutanguka kwa ukoloni, mataifa
walipopigania uhuru wa kujitawala wao wenyewe. Kipindi hiki ndicho
tulipo na baado cha endelea. Twajionea
wazi wazi jinsi mambo yanavyoenda, maovu kutukuzwa na wema kudhalilishwa.
Neno la Mungu linadharauliwa na kudunishwa peupe. Ulimwengu nao unakazania kuhalalisha maovu na kuilazimu
Kanisa kuhalalisha dhambi. Zaidi, watu wote hata watoto wanatambua na
kuzipigania haki zao ili wazimiliki nafsi zao wenyewe.
Hapa Kanisa limeadhirika pakubwa kwa
dhambi na kuwafanya wachungaji pamoja na viongozi wake wasiheshimike. Wale
wanaofuata desturi na itikadi za Kikristo wanachukuliwa kuwa wajinga na
washamba kupidukia, huku Kanisa likijibidiisha kufanana na ulimwengu kwa hali
na mali.
-Kanisa
lina jina la kuwa hai lakini limekufa.
-Matendo
yake yamekaguliwa na kupatikana si-timilifu mbele za Mungu.
-Bw.
Yesu analihimiza kutubu na kuimarisha mambo yaliyosalia kabla yaangamie.
-Hata
hivyo kuna wachache kati yao ambao hawajatia mavazi yao uchafu.
-Zaidi
ya hayo wanapewa onyo, wakeshe kwa kuwa Bwana atakuja kama mwizi bila hao
kukusudia!
-Aliyemsafi
atakwenda pamoja na Bw. Yesu na jina lake halitafutwa toka kitabu cha uzima
na Bwana atalikiri jina lake mbele za Mungu Baba na malaika wake.
SIKU YA TANO
(MWA. 1:20-23)
HISTORIA YA ULIMWENGU
KANISA LA SARDI
(UFU. 3:1-6).
Siku hii inafananishwa na
kipindi cha Madhila.
Kipindi hiki kimejaa ubishani,
fujo na mashindano. Kila mtu akitaka
kuitawala nafsi yake mwenyewe. Desturi za Ukristo hazi heshimiki wala kutambuliwa, uasi Mungu
umekidhiri mpaka ndani ya Kanisa. Wanadamu wanajishugulisha na haja zao za
mwili peke yake kwa hivyo dhambi imezidi
hata kupita mipaka. Kwa Kanisa, madhila makuu ya ungojea mwili wa
Kristo, maana, dhambi inatawala kote hata Kanisani jambo ambalo Mwenyezi atarekebisha
mwenyewe na kuutakasa Mwili wa Kristo na ulimwengu kwa hukumu za
kutisha.
Sawa na wanyama ambao Mungu aliwafanya katika siku hii,
kila mmoja huitawala nafsi yake na kuongozwa na tamaa zake. Ndivyo ulimwengu
ulivyo katika enzi hii.
Katika Agano la Kale kipindi hiki kilianza
na utawala wa Mfalme Manase. Utawala kuwa umejaa kila aina ya maovu na
madhila kiasi cha kumkasirisha Mungu. Kinpindi hiki kiliendelea hadi pale
wana wa Israeli walipoharibiwa na adui zao na kubebwa mateka hadi Babloni.
Kipindi hiki kilianza na vita vya Kwanza vya Dunia. Ambavyo vilichangia pakubwa kutanguka kwa ukoloni, mataifa
walipopigania uhuru wa kujitawala wao wenyewe. Kipindi hiki ndicho
tulipo na baado cha endelea. Twajionea
wazi wazi jinsi mambo yanavyoenda, maovu kutukuzwa na wema kudhalilishwa.
Neno la Mungu linadharauliwa na kudunishwa peupe. Ulimwengu nao unakazania kuhalalisha maovu na kuilazimu
Kanisa kuhalalisha dhambi. Zaidi, watu wote hata watoto wanatambua na
kuzipigania haki zao ili wazimiliki nafsi zao wenyewe.
Hapa Kanisa limeadhirika pakubwa kwa
dhambi na kuwafanya wachungaji pamoja na viongozi wake wasiheshimike. Wale
wanaofuata desturi na itikadi za Kikristo wanachukuliwa kuwa wajinga na
washamba kupidukia, huku Kanisa likijibidiisha kufanana na ulimwengu kwa hali
na mali.
-Kanisa
lina jina la kuwa hai lakini limekufa.
-Matendo
yake yamekaguliwa na kupatikana si-timilifu mbele za Mungu.
-Bw.
Yesu analihimiza kutubu na kuimarisha mambo yaliyosalia kabla yaangamie.
-Hata
hivyo kuna wachache kati yao ambao hawajatia mavazi yao uchafu.
-Zaidi
ya hayo wanapewa onyo, wakeshe kwa kuwa Bwana atakuja kama mwizi bila hao
kukusudia!
-Aliyemsafi
atakwenda pamoja na Bw. Yesu na jina lake halitafutwa toka kitabu cha uzima
na Bwana atalikiri jina lake mbele za Mungu Baba na malaika wake.
No comments:
Post a Comment